Taasisi ya huduma za macho ya Ujerumani
inayofahamika kama Tanzaneye imetoa misaada ya vifaa tiba, majengo na mafunzo
ya tiba ya macho wenye thamani ya Zaidi ya shilingi bilioni tatu kwa mikoa ya
Kigoma, Katavi na Rukwa nchini Tanzania. Mwandishi wetu Prosper Kwigize
ametuandalia ripoti ifuatayo
Akitoa taarifa katika hafla ya kukabidhi vifaa
tiba na uzinduzi wa ujenzi wa kituo kikubwa cha tiba ya Macho katika hospitali
ya Kabanga inayomilikiwa na Jimbo Katoliki la Kigoma, Mkurugenzi wa Tanzaneye
kutoka Bonn Ujerumani Dr. Karsten Paust amesema, taasisi hiyo iliyoanzishwa
mwaka 2017 inalenga kuunga mkono serikali na kanisa katoliki katika kutoa
huduma ya macho katika maeneo ambayo hayajafikiwa na taasisi nyingine
Paust amebainisha kuwa lengo la shirika hilo
linaloundwa na wajerumani na watanzania ni kusaidia nchi ya Tanzania kuongeza
idadi ya wataalamu wa afya ya macho kwa kutoa mafunzo ambapo tayari madaktari 45
wamejengewa uwezo
Akipokea misaada hiyo, Askofu wa jimbo katoliki la
Kigoma Joseph Mlola ameishukuru Tanzaneye kwa kukubali kushirikiana na kanisa
kuokoa afya ya macho kwa wananchi katika ukanda wa Ziwa Tanganyika na kuahidi
kuimarisha ushirikiano baina yao.
Kaimu mganga mkuu wa mkoa wa Kigoma Dkt. Ibrahim
Sahele amekiri kuwa mkoa huo una upungufu mkubwa wa vifaa tib ana wataalamu wa
huduma ya afya ya macho na kwamba ufadhili iliotolewa na tanzaneye umekuja kwa
wakati sahihi
Dkt Salehe anabainisha kuwa mkoa wa Kigoma pekee
una vituo vya kutolea huduma za afya Zaidi ya 300 vinavyokabiliwa na uhaba wa
vifaa tiba ya macho sambamba na miundombinu na anatoa wito kwa wadaua Zaidi kujitokea
kusaidia sekta hiyo
Akizungumza kuhusu takwimu, Mratibu wa TanzanEye
nchini Tanzania Bw. Ryner Linuma anaeleza kuwa kiwango cha magonjwa ya macho
nchini Tanzania kinafikia asilimia 4 ya wagonjwa wote na kwamba juhudi
mbalimbali zinahitajika ili kuondoa uwezekano wa wagonjwa kupata upofu
Linuma anabainisha kuwa changamoto kubwa ya macho
nchini Tanzania ni tatizo la mtoto wa jicho ambalo linafikia asilimia 70 ya
magonjwa yote ya macho nchini Tanzania
Akihutubia katika hafla hiyo kaimu Katibu tawala
wa mkoa wa Kigoma Bw. Elisante Mbilo amekiri kuwa serikali inahitaji wadau Zaidi
katika kuboresha huduma za afya hasa katika maeneo ya vijijini
Jumla ya vituo vya huduma za afya ya macho 18 ikiwemo
hospitali za halmashauri za wilaya ya Kakonko, Kibondo, Uvinza, Buhigwe, Kasulu
na Halmashauri ya Mji wa Kasulu zimepata msaada wa vifaa tiba ya macho kutoka
TanzanEye ya Ujerumani
0 Comments