Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Maweni – Kigoma imeendelea kutoa huduma ya upasuaji kwa mgonjwa mwenye tatizo la nyonga ikiwa ni siku ya tano ya kambi ya matibabu ya kibingwa na Ubingwa Bobezi katika hospitali hiyo.
Akizungumza na waandhishi
wa habari Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt Joseph Nangawe amesema
wananchi hawanabudi kufika kupata huduma hiyo kwasababu wataalamu wanatoa
huduma bora na ya umakini kwa wagonjwa.
“Hospitali na timu
nzima ya upasuaji imefanya mandalizi ya kutosha kwanzia kuingia hospitali,
hivyo niwahakikishie wananchi kuwa huduma hii ni salama lakini pia niendelevu
na leo niupasuaji wa kwanza wa nyonga katika hospitali yetu” amesema Dkt
Nangawe, Kaimu Mganga Mfawidhi.
Aidha Dkt Nangawe ameongeza kuwa Serikali imeendelea kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kwa kuwapeleka madaktri Bingwa na Bobezi katika hospitali za kanda Pamoja na hospitali za rufaa ambao wanasaidia kutoa huduma kwa wananchi.
“Hizi ni jitihada
za Serikali yetu ya awamu ya sita ambayo imekuwa ikileta madakitari Bingwa na
Bobezi katika hospitali zetu za rufaa kwa lengo la kuwasaidia wangonjwa katika
magonjwa mbalimbali hii ndiyo sababu ya hiki kinacho fanyika hapa leo” amesema
Dkt Nangawe.
kwa upande wake Dkt
Wilson Masanja ambaye ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya mifupa kutoka Hospitali
ya Kanda Bugando Mwanza amesema, katika kambi hiyo ya siku tano huduma ya kubadilishia
nyonga kwa mgonjwa ambaye amesumbuliwa na tatizo hilo kwa muda mrefu imefanyika
huku akitoa wito kwa wananchi kutumia Hospitali ya Maweni kupata huduma hizo.
“Mala nyingi
huduma hizi ninapatikana katika hospitali kubwa za kanda lakini leo
tumefanikiwa kufanya upasuaji huu mkubwa hapa, niupasuaji wa kwanza hapa Maweni
hivyo wananchi wafike kupata huduma kwa sababu huduma hizi kuzifuata katika hospitali
zinazotoa huduma hizi moja kwa moja ni gharam kubwa kuliko hapa” amesema Dkt
Masanja.
Kwa mujibu wa Dkt
Wilson Masanja ambaye ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya mifupa kutoka Hospitali
ya Kanda Bugando Mwanza amesema Upasuaji wa kubadilisha nyongwa kwa wangonjwa
waliokuwa wanasumbuliwa na tatizo hilo kwa muda mrefu umefanyika katika
hospitali ya Rufaa ya Maweni na umefanikiwa kwa asilimia 100.
Mwandishi. Halfani Rajabu
0 Comments