Kila mwananchi Burundi atamiliki faranga milioni moja 2027

 

Rais wa Burundi atangaza mkakati wa kila Mrundi anamiliki kiasi cha Faranga MILIONI 1 ifikapo mwaka 2027kama sehemu ya mkakati wa chama tawala nchini humo kuwezesha jamii kumiliki uchumi na kutokomeza umasikini wa kipato

Akihutubia katika mkoa wa Ngozi kwenye uzinduzi wa kampeni za chama tawala kuwania kushika hatamu ya Udiwani na Ubunge katika uchaguzi utakaofanyika june 5 mwaka huu, Rais Ndayishimiye amebainisha kuwa kupitia kilimo cha mahindi, mpunga, mbogamboga na matunda umasikini utakoma na kila mwananchi atakuwa na kipato.

Mheshimiwa Ndayishimiye amekiri kuwa kupitia misimamo ya chama na maelekezo ya kitaalam kwa wananchi, Nchi ya Burundi imefanikiwa kukomesha njaa na kwamba sasa ni kusaka pesa na kujenga makazi bora ili kila mwananchi aepukane na kuishi kwenye nyumba za nyasi

Aidha Rais Ndayishimiye pia ametumia kampeni hizo kutangaza mkakati wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kwa kutangaza mpango wa kila mwananchai kutumia gesi safi ya kupikia na kupunguza kiwango cha matumizi ya kuni na mkaa kwa ajili ya upishi. 

Ameeleza kuwa serikali ya Burundi Tayari imeweka mkakati madhubuti wa kusambaza gesi na kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala ili kupunguza au kukomesha uharibifu wa mazingira unaotokana na ukatazi wa miti kwa ajili ya kuni na mkaa

Maelfu ya raia wa Burundi wamehudhuria kampeni za chama tawala cha CNDD-FDD mkoani Ngozi

Katika hatua nyingine Raia wa Burundi wanaoishi nje ya bara la afrika maarufu Diaspora wametangaziwa neema kufuatia Katibu mkuu wa chama cha CNDD FDD Bw. Reveren Ndikuliyo pamoja na Rais Ndayishimiye kwa pamoja kutangaza mpango wa kuwapa nafasia ya uanzishaji wa miradi ya kimkakati utakaorahishwa na serikali ijayo itakayowapa ardhi bila kusumbuliwa na ametumia hotuba yake kutoa maelekezo kwa idara inayohusika na uwekezaji kuwapa kipaumbele Diaspora wanapoomba vibali na ardhi kwa ajili ya uwekezaji

Wakati huo huo chama tawala nchini Burundi kumejigamba kufanikisha mkakati wa kuiunganisha Burundi na nchi ya Tanzania na DRC kupitia katika mpango wa ujenzi wa Reli ya kisasa SGR ambayo ujenzi wake umeanza kutoka Kigoma nchini Tanzania kwenda Bujumbura na Uvira kupitia mkoa wa Rutana na Gitega

Katibu mkuu wa CNDD-FDD akihutubia maelfu ya wananchi na wafuasi wa chama hicho mkoani Ngozi kwenye uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mkuu wa madiwani na Wabunge 2025

Katibu mkuu wa CNDD_FDD amesisitiza kuwa chini ya mpango huo wa kuinua sekta ya usafirishaji, Jiji la Bujumbura litajengewa mfumo wa reli ya kisasa kwa ajili ya usafiri na utalii katika jiji hilo kubwa la kibiashara nchini Burundi


Kampeni za Uchaguzi mkuu wa wabunge, na madiwani zinatangulia miaka miwili kabla ya uchaguzi mkuu wa Rais utakaofanyika July 2027 kufuatia mabadiliko yaliyofanywa katika katiba ya Burundi, ambapo awali chaguzi zote zilifanyika kwa wakati mmoja

Prosper Kwigize

CA, Ngozi Burundi

Post a Comment

0 Comments