Prof. Ndalichako awagusa wajasiriamali soko la Sofya Kasulu akinadi Ilani


Mgombea Ubunge Jimbo la Kasulu Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Prof. JOYCE NDALICHAKO  amewashukuru wananchi wa Jimbo hilo kwa kujitokeza siku ya kampeni za Dkt. Samia Suluhu Hassan mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM siku ya Sept. 13 Wilayani Kasulu.

Shukurani hizo amezitoa alipotembelea Soko la Sofya lililopo Kasulu Mjini na kuwapongeza wananchi kwa namna wanavyounga mkono juhudi za Serikali ya CCM kwa kufanya biashara na kujiongezea kipato na kuwahimiza kuendelea kukiamini Chama Cha Mapinduzi CCM  kwa Awamu nyingine. 

Profesa Ndalichako ameelezea mafanikio mbalimbali yaliyopatikana katika kipindi chake cha Ubunge 2020-2025 akitaja kuboreshwa kwa mazingira ya kibishara katika soko la Sofya, Mikopo kwa wajasiriamlai, Ujenzi wa Shule mpya za msingi na sekondari pamoja na sekta ya afya

Profesa Joyce Ndalichako akiteta na kufurahia jambi na wafanyabiashara wa dagaa katika soko la Sofya mjini Kasulu akielekea katika harakati za kunadi Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa ajili ya Uchaguzi mkuu 2025
 

Ametaja kuendelea kuimarika kwa miundombinu ya barabara mjini Kasulu huku akibainisha kuwa serikali mpya ya CCM itakapoingia madarakani imejipanga kufanya mambo makubwa Zaidi kwa wakazi wa jimbo la Kasulu mjini.

Aidha Prof. NDALICHAKO amewaomba wananchi kujitokeza siku ya Uchaguzi kwa ajili ya kumpigia kura Dkt. Samia Suluhu Hassan, Madiwani wote wa jimbo la Kasulu Mjini na Kasulu Vijijini Pamoja na Jina La Joyce Ndalichako.

 

Profesa Joyce Ndalichako (Mgombea Ubunge Jimbo la Kasulu Mjini) akinunua mchele kwa wafayabiashara wanawake katika soko la Sofya mjini Kasulu ambako alitembelea kunadi sera za Chama cha Mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa wa Oktoba 29 mwaka huu

Profesa Ndalichako amekuwa Mbunge wa Kasulu mjini katika Kipindi cha 2020-2025 na awali alikuwa mbunge wa kuteuliwa kati ya Mwaka 2015-2020 na alishika nafasi za uwaziri wa elimu na Uwaziri wa Kazi kwa vipindi mbalimbali.

Jimbo la Kasulu Mjini ni miongoni mwa majimbo mawili yaliyopo katika wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma.

Kwa Mujibu wa Kanuni za tume huru ya taifa ya uchanguzi INEC Uchaguzi mkuu umepangwa kufanyika Octoba 29 mwaka 2025 kwa kuwachagua viongozi mbalimbali kuanzia Madiwani, Wabunge na Nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

Post a Comment

0 Comments