Maelfu ya raia wa Burundi wamejitokeza jana kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa Wabunge na Madiwani huku amani ikitawala katika vituo vyote vya kupigia kura na katika mitaa mbalimbali nchini humo.
Buha
News imezuru katika tarafa kadhaa za mkoa wa Burunga ambao awali ulitambulika
kama Makamba, Tutana na Gitega ambayo ni makao makuu ya nchi na kushuhudia
makundi makubwa ya wananchi wakipanga mstari kuelekea vyumba vya kupigia kura
kwa amani.
Wakizungumza
kabla na hata baada ya kupiga kura wananchai na viongozi wamekiri kuwa uchaguzi
umeandaliwa vizuri na kwamba hakuna aliyekosa jina lake kwenye orodha ya wapiga
kura na kwamba wana matumaini na uchaguzi ulio huru na haki
Je!
Ni matarajio gani ya wananchi hususani katika mikoa ya pembezoni na vijijini
baada ya kumalizika kwa uchaguzi huu, wengi wa wananchi wanakiri kuwa licha ya
nchi hiyo kufanikiwa kushughulikia changamoto za ulinzi na usalama jitihada
zinahitajika kwenye miundombinu. Mama huyu ni mmoja wa maelfu ya wanawake
waliojjitokeza kutekeleza wajibu wao wa kikatiba
Bw.
Sinzinkayo Sylvester ni mwangalizi wa ndani wa uchanguzi huo matika mkoa wa
Makamba, kwa upande wake anaeleza kuridhishwa na taratibu zilizoandaliwa na
Tume huru ya uchaguzi nchini Burundi CENI na kuweka bayana kuwa hana sshaka
kwamba kila mwananchi mwenye sifa na aliyejiandikisha atapata haki yake
Katibu
mkuu wa chama tawala cha CNDD-FDD Ndikiriyo Reverie ni mmoja wa wananchi
waliojitokeza kupiga kura katika kituo cha shule ya msingi Sampeke iliyopo
katika kijiji cha Nyantakara wilayani Kayogoro alikozaliwa, pamoja na
kuridhishwa na mwamko wa wananchi kujitokeza kupiga kura anaamini kuwa chama
chake kitashinda
Uchaguzi
wa Madiwani na wabunge 2025 unatangulia uchaguzi wa Rais utakaofanyika mwaka
2027 kufuatia mabadiliko ya Katiba ya Burundi inayompa Rais kipindi cha miaka
saba ya kuongoza tofauti ya miaka miwili ya wabunge na madiwani.
Hadi sasa amani imetawala nchini kote na wananchi wanaendelea na majukumu yao kama kawaida wakisubiri kutangazwa kwa matokeo rasmi ya nani kashinda ambayo yanatarajiwa kutangazwa na tume huru ya uchaguzi nchini Burundi CENI wakati wowote kuanzaia sasa.Tumedhamiria kujenga nchi yetu kidemokrasia, tunataka Burundi ifikie uchumi wa kati ifikapo 2040. Wananchi wanadhamira hiyo kupitia karatasi ya kupigia kura. Anasema Katibu Mkuu wa Chama cha @CnddFdd ndugu @R_Ndikuriyo baada ya kupiga Kura mkoani Burunga pic.twitter.com/29q9SgKU0X
— Prosper Laurent. Kwigize (Baraka) (@PeaceTanzania) June 5, 2025
Mufti wa Burundi Salum Nayabagabo atumia ibada ya Eid el Adha kukipongeza chama cha @CnddFdd kwa kupata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa wabunge na madiwani. Katibu mkuu @R_Ndikuriyo awashukuru wananchi wa dini zote kwa ushirikiano. Matokeo rasmi kutangazwa wakati wowote pic.twitter.com/AJ6wqfTvGt
Taarifa zisizo rasmi zinataja kuwa chama tawala cha CNDD-FDD kinaongoza katika matokeo ya awali na huenda kikapata ushindi wa zaidi ya 90% na hivyo kuwa na uhakika wa kuunda serikali.
Imeandikwa na. Prosper Kwigize
Bujumbura,
Burundi
0 Comments