Kocha Mkuu wa Man Utd Erick ten Hag amelaani makosa ya kiakili ambayo yalichangia kufungwa kwa kikois chake dhidi ya Galatasaray ya Uturuki katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya uliochezwa juzi Jumanne (Oktoba 03).
Mashetani Wekundu walikuwa mbele mara mbili wakati wa nchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Old Trafford, lakini hatimaye walipoteza 3-2 baada ya makosa kadhaa ya safu ya ulinzi ikiwa moja la Andre Onana na kumfanya Casemiro kuonyeshwa kadi nyekundu kwa kucheza rafu eneo la hatari.
Kipigo hicho kilikuwa cha sita kwa United katika msimu huu ambao umekuwa mbaya zaidi hadi sasa, na klabu hiyo iko mkiani katika kundi lake baada ya kufungwa mechi zao mbili walizocheza.
0 Comments